cellcom-prcd-rencrontre-deux-presidents

Baada ya Mkataba wa Amani Washington: Nini Kifuatavyo kwa Rwanda na DRC?

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Rwanda zilitia saini mkataba wa amani uliosimamiwa na Marekani tarehe 27 Juni 2025 huko Washington DC.
Wakati bado kunasubiriwa kutiwa saini kwa makubaliano kati ya viongozi wa Congo na kundi la AFC/M23 huko Doha, je, nini kinafuata baada ya makubaliano ya Washington?

Hatua ya kwanza kabla ya 27 Julai 2025:

Rwanda na DRC lazima ziunde mfumo wa uratibu wa pamoja, utakaoambatana na kamati ya ufuatiliaji inayojumuisha Umoja wa Afrika (AU), Marekani, na Qatar.
Mkutano wake wa kwanza unapaswa kufanyika kufikia tarehe 11 Agosti.

Kwenye ardhi, mambo mawili ya haraka:

  1. Kulivunja kundi la waasi la FDLR (linalopinga serikali ya Rwanda)

  2. Kuondoa hatua za ulinzi zilizowekwa na Rwanda

Hatua hizi zinapaswa kukamilika ndani ya miezi minne, kwa awamu kadhaa.

Miezi mitatu ya kuivunja FDLR

Awamu ya kwanza itakuwa ya wiki mbili za maandalizi, kuchambua taarifa, kutambua wapiganaji wa FDLR, na kubadilishana habari za kiusalama.

Kisha, operesheni ya miezi mitatu itaanza ya kuwasambaratisha FDLR na kuondoa ulinzi wa Rwanda.
Kwa mujibu wa RFI, operesheni ya pamoja ya FARDC na RDF inawezekana — lakini itahitaji makubaliano ya nchi zote mbili.

Kwa upande wa uchumi:

Kabla ya 27 Septemba, nchi hizo mbili zinapaswa kuanzisha mpango wa kuunganisha uchumi wa kikanda, hususan kuhusu raslimali, biashara na uwekezaji wa mipakani.

“Mapigano yanaweza kurudi wakati wowote”

Kundi la M23 halikualikwa kwenye mazungumzo ya Washington, licha ya kuanzisha tena vita mwishoni mwa 2021 na mwanzo wa 2022, na kuchukua maeneo mengi mashariki mwa DRC. Rwanda inashutumiwa kulisaidia, japo inakanusha.

Tatizo la AFC/M23 limepelekwa kwa mazungumzo ya Doha, yakilenga kufikia makubaliano ya moja kwa moja na serikali ya Kinshasa.

Akizungumza na RFI, Pierre Boisselet kutoka taasisi ya Ebuteli alisema kuwa makubaliano ya amani hayamaanishi kuwa vita vimekwisha, hata kama hali imeonekana kutulia hivi karibuni.

Alisema:

“M23 ni imara zaidi kuliko mwaka 2013. Wanadhibiti maeneo ya kimkakati. Inaonekana wamewekeza sana katika mafunzo ya kijeshi. Taarifa zinaonesha kuwa RDF ilikuwa mstari wa mbele katika mapambano. Hivyo, M23 haijathibitisha kuwa inaweza kupigana yenyewe dhidi ya FARDC.”

Sasa swali ni:

Je, DRC itatimiza ahadi zake za Washington, ikivunja uhusiano na kundi la FDLR ambalo imesaidia kwa muda mrefu?
Na nini kitaibuka katika mazungumzo ya Doha na AFC/M23?

Sangiza iyi nkuru

Soma Izindi Nkuru

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *