Mwanamitindo wa Uganda anayeishi London, Eva Apio, amekanusha uvumi kuwa yuko katika uhusiano wa kimapenzi na msanii maarufu kutoka Nigeria, Asake.
Alijibu tetesi hizo kupitia Twitter baada ya mtumiaji mmoja kumuita “mpenzi wa Asake.” Eva alimjibu moja kwa moja: “Sijawahi kuwa mpenzi wake.”
Kauli hiyo ya Eva imekuja baada ya watu wengi kuhoji kuhusu uhusiano wake na Asake, hasa kwa sababu wameonekana mara kadhaa pamoja kwenye hafla mbalimbali, ikiwemo Paris Fashion Week.
Hata hivyo, Eva alisisitiza kuwa hakuna uhusiano wa kimapenzi uliokuwepo kati yao, bali watu walitafsiri vibaya urafiki wao wa kawaida.




