e2dd1de0-0217-11ef-946e-d7e525632c0f

Huzuni Kubwa: Mshambuliaji wa Liverpool na Ureno Diogo Jota Afariki Ajali ya Gari

Alhamisi, Julai 3, mshambuliaji Diogo Jota, aliyekuwa akichezea Liverpool England na timu ya taifa ya Ureno, alifariki katika ajali ya gari.

Ajali hiyo pia imeua mdogo wake Andre Félipe, ambaye pia alikuwa mchezaji wa soka, karibu na Zamora nchini Uhispania.

Vyombo vya habari vya Uhispania vinaripoti kwamba wale kaka wawili walikufa papo hapo.

Jota, mwenye umri wa miaka 28, alifariki wiki mbili tu baada ya kuoa mchumba wake wa muda mrefu, Rute Cardoso, waliokuwa pamoja tangu 2012.

Alianza kazi yake ya soka nchini Ureno, kabla ya kuhamia Atlético Madrid Uhispania. Kisha alijiunga na Wolverhampton Wanderers Uingereza, na mwaka 2020 akahamia Liverpool.

Katika miaka mitano aliyotumia kwenye klabu hiyo ya Merseyside, aliisaidia kushinda mataji kadhaa, ikiwa ni pamoja na ubingwa wa Ligi Kuu msimu uliopita.

Sangiza iyi nkuru

Soma Izindi Nkuru

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *