Jumanne, Julai 8, Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC) ilitoa hati za kukamatwa kwa Kiongozi Mkuu wa Afghanistan chini ya utawala wa Taliban na Rais wa Mahakama Kuu yao, kwa tuhuma za kuwatesa wasichana na wanawake nchini Afghanistan.
ICC imesema kuna ushahidi wa kutosha kwamba Kiongozi wa Kiroho wa Taliban, Haibatullah Akhundzada, na Jaji Mkuu wa Taliban, Abdul Hakim Haqqani, walitenda uhalifu dhidi ya ubinadamu kwa kuwatesa watu kwa misingi ya kijinsia — hasa wasichana, wanawake, na wengine wanaopinga sera za Taliban kuhusu jinsia, utambulisho au maoni, kama ilivyobainishwa na Mahakama ya Umoja wa Mataifa.
“Wakati Taliban walipoweka sheria na vizuizi kwa wananchi wote, walilenga hasa wasichana na wanawake kwa sababu ya jinsia yao, na kuwakosesha haki na uhuru wao.”
![]()
Kiongozi Mkuu wa Afghanistan, Haibatullah Akhundzada
Majaji wa ICC walisema Taliban wame*“nyima vikali”* wasichana na wanawake haki zao za kupata elimu, faragha, maisha ya kifamilia, uhuru wa kusafiri, kuzungumza, kufikiri, dhamira na dini.
Taliban wamesemaje?
Mahakama hiyo yenye makao yake The Hague, imesema makosa haya yalitendeka kuanzia Agosti 15, 2021 (siku Taliban walichukua madaraka) hadi angalau Januari 20, 2025.
Katika taarifa yao, msemaji wa Taliban, Zabihullah Mujahid, alisema:
“Taliban wanapinga hati hizi za ‘ujinga’ za kukamatwa na wanasema kwamba uamuzi wa ICC hautaathiri juhudi zao kali na kujitolea kwa sheria ya kiislamu (sharia).”




