Gt37nS8XcAACCe5

Musanze: Maafisa Wakuu 34 wa Polisi Kutoka Afrika Wahitimu Mafunzo ya Uongozi

Katika Chuo Kikuu cha Polisi kilichoko Wilaya ya Musanze, siku ya Ijumaa tarehe 20 Juni 2025, ulifanyika sherehe ya kuhitimu kwa kundi la 13 la mafunzo ya mwaka mmoja kuhusu uongozi kwa maafisa waandamizi wa polisi (Police Senior Command and Staff Course).

Mwaka huu, maafisa waandamizi 34 kutoka nchi tisa za Afrika waliungana na wenzao wa Rwanda kusherehekea mafanikio ya kuhitimu mafunzo hayo ambayo yamechukua mwaka mzima.

Sherehe hiyo ilihudhuriwa na Waziri wa Usalama wa Ndani, Dkt. Vincent Biruta, pamoja na mabalozi na wawakilishi kutoka nchi zilizoshiriki.

Kamanda wa Chuo cha Polisi, Kamishna wa Polisi Rafiki Mujiji, alisema katika hotuba yake:

“Mafunzo ya uongozi tunayoyakamilisha leo ni ya mwaka mmoja, yakitolewa kwa ushirikiano kati ya Chuo cha Polisi, Chuo Kikuu cha Rwanda na African Leadership University. Tunafurahia kutangaza kuwa wanafunzi wote 34 wamehitimu kwa mafanikio. Mafanikio haya yanaonyesha bidii yao, nidhamu na kujitolea kwao. Mnaporejea kwenye taasisi zenu mbalimbali, tuna imani kuwa ujuzi na maarifa mliyojifunza yatawasaidia kukabiliana kwa taaluma na changamoto za kiusalama zinazotukabili leo.”

 

Sangiza iyi nkuru

Soma Izindi Nkuru

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *