photonews_11045847-132

Ubelgiji Wabadili Msimamo: Watahudhuria Mashindano ya Dunia ya Baiskeli Kigali 2025

Baada ya kutangaza awali kuwa haitashiriki Mashindano ya Dunia ya Baiskeli yatakayofanyika Kigali, Rwanda mwezi Septemba, Serikali ya Ubelgiji imebadili uamuzi wake.

Shirikisho la Baiskeli la Ubelgiji limethibitisha kuwa timu ya taifa itashiriki mashindano hayo, baada ya kuomba ruhusa kutoka kwa serikali ili kusafiri kwenda Rwanda.

Mkurugenzi wa shirikisho hilo, Nathalie Clauwaert, amesema kuwa maandalizi yote, ikiwemo tiketi za ndege, hoteli na vifaa vya wachezaji, yanaendelea kufanyika.

Uamuzi huu unakuja miezi mitatu baada ya Ubelgiji kusitisha uhusiano wa kidiplomasia na Rwanda, ikidai kuwa Rwanda inaunga mkono kundi la waasi la M23 linalopigana dhidi ya serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Ubelgiji pia ilikuwa miongoni mwa nchi zilizoongoza kupendekeza vikwazo vya EU dhidi ya Kigali.

Mashindano ya Dunia ya Baiskeli yamepangwa kufanyika kuanzia tarehe 20 hadi 29 Septemba 2025. Waendesha baiskeli mashuhuri kama Victor Loulergue na Hugo Boucher wanatarajiwa kuiwakilisha Ubelgiji.

Sangiza iyi nkuru

Soma Izindi Nkuru

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *