Msanii wa muziki kutoka Tanzania, Zuchu, anayefahamika sana kwa wimbo wake maarufu “Sukari” na ambaye yupo chini ya lebo ya WCB ya Diamond Platnumz, ametangaza kuwa hatafanya tena kazi na wasanii wa Kenya.
Tangazo hilo limetolewa baada ya Wakenya kadhaa kutuhumiwa kumdhalilisha na kumkashifu Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, hadharani.
Zuchu alisema:
“Siwezi kufanya kazi na Wakenya kwa sababu hawana heshima. Wamemdhalilisha kiongozi wetu wa taifa. Wanapaswa kuomba msamaha!”
Tukio hili limeibuka wakati ambapo kuna tensi kubwa kati ya Tanzania na Kenya, hasa baada ya baadhi ya wasanii wa Kenya kutoa nyimbo zinazokosoa uongozi wa Rais Samia, jambo ambalo halijawahi kutokea siku za nyuma.
Kauli ya Zuchu imezua mjadala mkali kwenye mitandao ya kijamii, ambapo baadhi ya Wakenya walimkejeli na wengine wakimkosoa vikali.




